HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

15 October 2013

UKATA WAIONDOA MALAWI KOMBE LA CHALENJI



Baraza la vyama vya soka Afrika mashariki na kati limepata pigo baada ya timu mwalikwa maarufu kama mware wa Nyasa ,Malawi kujitoa katika michuano hiyo ya Chalenji baada ya kukosa fedha za kuendesha timu hizo .

Jambo hili linakuja baada ya Nchi hiyo kusimamisha shughuri zote za kimaendeleo ya soka kwa timu za vijana na wakubwa kwa ukosefu wa pesa.

Michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Nov 27 na kumalizika Dec 12 nchini Kenya .

Mapema wiki hii ,Katibu mkuu wa Cecafa Nicholas Musonye ametangaza kuwa Cote d’Ivoire haitashiriki michuano kutokana na matatizo ya kiuchumi

Kwa maana hiyo timu ya vijana ya malawi chini ya miaka 20 haitashiriki michuano hiyo itakayofanyika Lesotho mwishoni mwa mwaka huu .

Rais wa Chama soka cha malawi  Walter Nyamilandu, ambaye alinukuliwa na chombo cha cha habari cha nchi hiyo ,Hwajapokea mwaliko kutoka Cecaafa na hata wakipokea hawatoshiriki kwani hawana pesa  .

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers